"UCHAGUZI UTAFANYIKA KWA UTULIVU NA AMANI" DKT SAMIA

 

"UCHAGUZI  UTAFANYIKA KWA UTULIVU NA AMANI" DKT SAMIA

"UCHAGUZI  UTAFANYIKA KWA UTULIVU NA AMANI" DKT SAMIA

DODOMA

Rais wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amesema serikali imejipanga katika kuhakikisha uchaguzi utafanyika katika mazingira ya utulivu na  amani ifikapo mwezi Oktoba mwaka huu.

Rais Samia ametoa kauli hiyo April 25, 2025 wakati akilihutubia Taifa kupitia vyombo vya habari Ikulu  ya Chamwino Ikiwa ni siku moja kuelekea  miaka 61 ya  Muungano tarehe 26, April.

"Tutafanya kila tuwezalo kuhakikisha kuwa uchaguzi unafanyika kwenye mazingira ya utulivu na amani katika kipindi chote cha matayarisho hadi wakati  wa uchaguzi ili kuwa na uchaguzi huru na wa haki"Amesema Mhe.Rais Samia

Aidha Mhe.Rais Dkt Samia ametoa wito kwa wananchi  kujitokeza kushiriki katika mchakato  mzima wa uchaguzi kuanzia kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura, kugombea hadi kupiga kura .

Vilevile  Mhe. Rais Samia amewataka viongozi, wanachama na wafuasi wa vyama vya  siasa kuzingatia taratibu na sheria za nchi ili uchaguzi huu uwe  fursa ya kuimarisha umoja  na demokrasia ili tupate viongozi  walio  bora na  imara.

#MIAKA61YAMUUNGANO