TSH BIL 88.725 ZINAJENGA KM 50 KIBAONI-MLELE

 

TSH BIL 88.725 ZINAJENGA KM 50 KIBAONI-MLELE

TSH BIL 88.725 ZINAJENGA KM 50 KIBAONI-MLELE

KATAVI
Kiasi cha shilingi bilioni 88.725 kinatekeleza ujenzi wa barabara  ya Kibaoni – Sitalike, sehemu ya kwanza ya Kibaoni – Mlele (km 50) kwa kiwango cha lami  katika Halmashauri ya Mpimbwe  mkoani Katavi.
Miradi mingine inayoendelea  kutekelezwa  katika Hlamshauri hiyo ni  Barabara Vikonge – Luhafwe (km 25) ambao upo 57.4%  na unagharimu Sh bilioni 35.6, barabara ya Luhafwe – Mishamo (km 37) upo 10%  ya utekelezaji na unagharimu Sh bilioni 58.3 pamoja na barabara inayoelekea Bandari ya Karema kutoka Kagwira zaidi ya kilometa 112 Mkandarasi ameshapatikana na mwaka huu barabara hiyo itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami.
#TukutaneKatavi