MHE.RAIS SAMIA ASAMEHE WAFUNGWA 4887

 
MHE.RAIS SAMIA ASAMEHE WAFUNGWA 4887

MHE.RAIS SAMIA ASAMEHE WAFUNGWA 4887 

MHE.RAIS SAMIA ASAMEHE WAFUNGWA 4887 

DODOMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa msamaha kwa wafungwa  4887 ambapo  42 kati yao wanaachiliwa huru leo  tarehe 26 April na wengine  4845 wanabaki gerezani kumalizia sehemu ya kifungo kilichobaki  baada ya kupewa msamaha huu.


Msamaha huu umewahusu wafungwa wa makundi mbalimbali ikiwemo:-
a. wafungwa wagonjwa wenye magonjwa  ya kudumu  au sugu ambao wapo kwenye hatua ya mwisho

b. wafungwa wote waliohukumiwa na mahakama kutumikia vifungo vya maisha gerezani wabadilishiwe vifungo vyao na kuwa vifungo  vya miaka 30 kuanzia tarehe ya hukumu (wafungwa hao wawe wamekaa gerezani kwa miaka mitano na kuendelea kuanzia tarehe ya hukumu)

c. Wafungwa waliohukumiwa kunyongwa na kumaliza taratibu za kimahakama wabadilishiwe adhabu ya kifo na kuwa kifungo cha maisha.

d. wafungwa wazee wenye umri wa miaka 70 au zaidi ambao wamehukumiwa kifungo cha muda maalum /ukomo  na waliokaa gerezani kwa muda wa miaka miwili   na  kuendelea.

e.  Wafungwa wa kike walioingia na mimba gerezani au wenye watoto wanaonyonya

f. Wafungwa wenye  ulemavu wa mwili na afya ya akili wasio na uwezo  wa kufanya kazi 

g.Wafungwa waliohukumiwa adhabu ya kuwekwa kizuizini ambao wamekaa gerezani kuanzia miaka 10 au  zaidi 

h. Wafungwa wakike wasionyonyesha na walioko gerezani

i. Wafungwa wenye ulemavu wa  akili

Aidha Msamaha huo HAUHUSISHI WAFUNGWA WAFUATAO
a.Wafungwa waliopatikana  na hatia na kuhukumiwa kifungo gerezani kwa makosa ya uhujumu uchumi,matumizi mabaya ya madaraka,utakatishaji wa fedha, rushwa na usafirishaji au kujihusisha kwa namna yoyote ile na madawa ya kulevya ikiwemo bangi

b. wafungwa waliopatikana na hatia na kuhukumiwa kifungo gerezani kwa makosa ya utekaji au wizi wa watoto,kupoka, kuwapa mimba wanafunzi na makosa yote yanayohusiana na ukatili kwa watoto na kujihusisha  kwa namna yoyote ile na biashara haramu ya binadamu.

c. wafungwa waliopatikana na hatia na  kuhukumiwa kifungo gerezani kwa makosa ya kukutwa na viungo vya binadamu, unyang'anyi wa kutumia nguvu/ silaha,kumiliki silaha,risasi,milipuko au kujaribu kutenda makosa hayo.

d.Wanaotumikia vifungo gerezani kwa makosa ya kujihusisha kwa namna yoyote ile na nyara za serikali au ujangili

e. Wanaotumikia vifungo gerezani kwa makosa ya wizi au ubadhilifu wa fedha za serikali 

f. Wanaotumikia vifungo kwa makosa ya kutoroka au kujaribu kutoroka chini ya ulinzi halali au kusaidia kutendeka kwa makosa hayo.

g. Wenye makosa ya kuua watoto wachanga, ugaidi,uharamia na makosa  ya kimtandao 

h. wanaotumika kifungo cha pili na warudiaji

i. Waliotenda makosa ya kinidhamu gerezani ambao makosa yao hayajatimiza mwaka mmoja mpaka kufikia april 26,2025

J. Wafungwa wa madeni

MUHIMU:- Kwa mamlaka aliyopewa chini ya Ibara ya 45 (1) (a) -(d) ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inamruhusu  Mhe. Rais kutoa msamaha huo na hatua hii ni katika kuadhimisha miaka 61 ya Muungano wa Tanzania tarehe  26 April 2025.