BIASHARA TANZANIA NA UBELGIJI KUONGEZEKA
TANZANIA
Tanzania inatarajia kukuza biashara na Ubelgiji baada ya hivi karibuni kuwakaribisha kwenye kongamano wawakilishi kutoka kampuni za Ubelgiji zinazotafuta fursa za biashara na uwekezaji nchini.
Kupitia kongamano hilo lililowezesha majadiliano kati ya serikali na ushirikishwaji wa biashara, lilitoa jukwaa kwa wananchi wa nchi zote mbili kuimarisha ushirikiano na kuunda uumoja katika sekta muhimu za kiuchumi kama vile kilimo na biashara.
Hafla hiyo ilileta pamoja wawakilishi kutoka makampuni 40 ya Ubelgiji na zaidi ya makampuni 350 ya ndani na kuwawezesha kujadili na kutafuta fursa za biashara na uwekezaji nchini Tanzania.
Aidha jukwaa hilo linaendana na juhudi kubwa za serikali ya awamu ya sita za kukuza uwekezaji, kufikia uchumi wa viwanda, kutengeneza ajira, kukuza teknolojia na kusukuma maendeleo ya uchumi wa nchi.
