MTANDAO WA BARABARA KM 109 KUFUNGULIWA

 

MTANDAO WA BARABARA KM 109 KUFUNGULIWA

MTANDAO WA BARABARA KM 109 KUFUNGULIWA 

MANYARA
Serikali  kupitia Wakala  wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoa wa Manyara ina mpango wa kufungua barabara mpya zenye urefu Km. 109 katika Wilaya ya Mbulu, Simanjiro pamoja na Babati  katika mwaka wa fedha  2024/2025.
Barabara zitakazofunguliwa ni zilizopo katika wilaya  ya Mbulu (Km. 46), Simanjiro (Km. 41), pamoja na Babati (Km. 22).
Pamoja na ujenzi wa km 109 pia serikali itajumuisha ujenzi wa barabara za lami(Km. 11.7),changarawe (Km. 251.4) pamoja na matengenezo ya barabara za udongo (Km. 385) na ujenzi wa vivuko vipatavyo 104.
Licha ya kufungua kilomita hizo za barabara hali ya mtandao wa barabara katika maeneo mengi katika mkoa huo ni nzuri kwani unapitika katika kipindi chote cha mwaka.