TSH MIL 800 ZAWAPATIA HOSPITALI NYASA

 

TSH MIL 800 ZAWAPATIA HOSPITALI NYASA

TSH MIL 800 ZAWAPATIA HOSPITALI NYASA

Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan  imetoa  shilingi milioni 800  ili kujenga Hospitali ya wilaya Nyasa iliyopo Mkoani Ruvuma lengo likiwa ni kusogeza na kuboresha huduma za afya kwa wananchi ambao awali walilazimika kwenda nje ya wilaya hiyo kufuata matibabu.
Hospitali ya Wilaya ya  Nyasa inatoa huduma zote muhimu kwa wananchi wa Mbambabay na wilaya  ya Nyasa kwa ujumla.
Kabla ya hospitali hiyo wananchi  wa wilaya ya Nyasa walikuwa wanasafiri umbali wa zaidi ya kilometa 66  kufuata huduma za matibabu katika Hospitali ya Mbinga.