KM 2,779 ZA MKONGO WA TAIFA ZAJENGWA
TANZANIA
Katika mwaka 2023/2024, Serikali imeendelea na ujenzi wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano ambapo hadi kufikia Machi, 2024 jumla ya kilomita 2,779 za Mkongo zimejengwa pamoja na vituo 111 vya kati vya mawasiliano.
Pia, imesambaza mkongo kwenye Wilaya 21 za Rorya, Nachingwea, Ludewa, Newala, Rombo, Same, Mwanga, Hai, Meru, Nanyumbu, Tandahimba, Muheza, Mkinga, Mkuranga, Tunduru, Namtumbo, Mbozi (Vwawa), Ngara, Kyela, Pangani na Muleba.
Vilevile, Serikali imeimarisha njia za ndani ya nchi kwa ajili ya ujenzi wa Mkongo wa Taifa kuunganisha na nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.