TSH BIL 69.243 ZAJENGA YADI & SAKAFU BANDARI YA KWALA

 

TSH BIL 69.243 ZAJENGA YADI & SAKAFU BANDARI YA KWALA

TSH BIL 69.243 ZAJENGA YADI & SAKAFU BANDARI YA KWALA

PWANI
Serikali imeendelea na ujenzi wa yadi na sakafu ngumu yenye ukubwa wa hekta tano katika Bandari Kavu ya Kwala  kwa ajili ya kuhifadhi shehena za mizigo, pia imekamilisha ujenzi wa  barabara ya zege yenye urefu wa kilomita 15.5 kutoka barabara kuu ya Morogoro hadi Bandari Kavu ya Kwala iliyopo katika mkoa wa Pwani ambapo utekelezaji  wa mradio huo umetumia shilingi bilioni 69.243.