TSH BIL 174.3 ZAWEZESHA RUZUKU YA MBOLEA
DODOMA
Jumla ya Shilingi Bilioni 174.3 zilitengwa kwa ajili ya kutoa ruzuku ya mbolea na kupima afya ya udongo katika mashamba mapya 30 yenye ukubwa wa hekta 200,000.
Mikoa iliyonufaika na mpango huo ni Pwani (hekta 60,000), Morogoro (hekta 50,000), Njombe (30,000), Songwe (hekta 30,000) na Tanga (hekta 30,000).
