LUDEWA WANA MIRADI 10 YA TSH BIL 25
NJOMBE
Wilaya ya Ludewa Mkoani Njombe inatekeleza miradi 10 yenye thamani ya shilingi bilioni 25 inayohusisha ujenzi wa miundombinu mbalimbali kwenye sekta ya Elimu, Afya pamoja na miundombinu ya Barabara na Maji
Pamoja na hayo pia Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan amelipa fidia ya shilingi Bilioni 15 kwenye mradi mkubwa wa Kitaifa wa Mchuchuma na Liganga ambao upo katika kijiji cha Mundindi , Kata ya Mundindi tarafa ya Liganga, wilayani Ludewa Mkoani Njombe.
