TANZANIA NA UTURUKI ZATILIANA SAINI HATI ZA MAKUBALIANO
UTURUKI
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Uturuki zimetiliana saini hati za makubaliano kufuatia ziara ya kiserikali ya Mhe Rais Samia inayoendelea katika nchi ya Uturuki kuanzia April 17 mwaka 2024.
Hafla ya utiaji saini imeshuhudiwa na Rais Samia Suluhu Hassan na Rais Recep Tayyip Erdoğan pamoja na mwakilishi wa Tanzania kutoka Kituo cha Uwekezaji (TIC) na mwakilishi wa Uturuki ambaye ni Makamu wa Rais wa Ofisi ya Rais Uwekezaji ya Jamhuri ya Uturuki Zeynel Kilınç.
Vilevile Mhe Rais Dkt Samia ameshuhudia utiaji saini hati za makubaliano kwa ajili ya kuanzisha ufadhili kwa wanafunzi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Mafunzo ya Amali wa Zanzibar na Serikali ya Uturuki wanaohitimu katika Elimu ya Juu
