RIPOTI- DKT SAMIA MICHEZONI KWA MIAKA MITATU

 

RIPOTI- DKT SAMIA MICHEZONI  KWA MIAKA MITATU

RIPOTI- DKT SAMIA MICHEZONI  KWA MIAKA MITATU

Wakati ikibaki siku moja kabla  ya   Mhe Rais  Dkt Samia  kutimiza  miaka  mitatu   ya uongozi wake (Machi 19,2021 –Machi 19,2024) BimkubwaTanzania inakuonesha ni kwa namna  gani  serikali  ya  awamu  ya  sita  imekuwa  ikigusa  moja  kwa  moja  sekta ya michezo
Ndani ya kipindi ch miaka mitatu, Mhe Rais Dkt Samia amejitanabaisha kuwa mdau mkubwa wa sekta ya michezo  kutokana na ushiriki  wake  katika  shughuli  mbalimbali za sekta hiyo  pamoja  na  mipango  mbalimbali ambayo uongozi wake umeiweka ili kuhakikisha michezo inapiga hatua Nchini.
Ushiriki Dkt Samia katika  michezo  umeonekana  kujenga  imani ya wengi kuwa huenda sekta  ya  michezo  ikapata  mafanikio  makubwa chini ya utawala wake,
Ipo mifano na uthibitisho wa wazi unaoonesha jinsi Rais Samia anavyotamani      kuona michezo sio tu inakuwepo kwa ajili ya kujifurahisha bali kugeuka fursa  ya  ajira na kukuza uchumi wa nchi.
UDHAMINI SOKA LA WANAWAKE CECAFA
Agosti 21, 2021, Rais Samia alikubali  ombi  la  Shirikisho  la  Soka  Tanzania  (TFF)  la  kuwa  mdhamini  wa  mashindano ya wanawake ya Cecafa.
SERENGETI GIRLS NCHINI INDIA KOMBE LA DUNIA LA FIFA 2022 :- Serikali ya awamu ya sita  ilichukua jukumu kubwa katika kuunga mkono timu ya Serengeti girls (U-17), kuwezesha kambi ya makazi katika nchi ya England( Nje ya Nchi ambayo mashindano yalikuwa yakifanyika)  ambapo walishiriki katika mfululizo wa mechi za maandalizi kuelekea michuano kufanikisha  kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia la FIFA 2022 nchini India.
TEMBO WARRIORS KATIKA KOMBE LA DUNIA LA AMPUTEE 2022, UTURUKI :- Kujitolea kwa Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika michezo kuliwezesha timu  ya  Taifa ya Soka kwa Walemavu, (Tembo Warriors)  kuweka kambi ya makazi ndani na nje ya nchi, kuelekea ushiriki wa timu hiyo kuwa miongoni mwa timu 24 zilizoshiriki katika hatua ya 16/17 ya Kombe la Dunia lililofanyika Istanbul, Uturuki, kuanzia Septemba 30 hadi Oktoba 9,  2022.
KUNUNUA KILA GOLI MECHI ZA KIMATAIFA :- Utawala  wa  Rais  Samia  mwaka 2022, ulianzisha utaratibu wa kuzipa hamasa  klabu  za  Tanzania  zilizokuwa  zinashiriki  mashindano  ya  klabu  Afrika  kwa  kutoa  kiasi  cha  Sh  5  milioni  kwa  kila  bao  ambalo  zilikuwa  zinafunga kuanzia hatua ya makundi na kuendelea.
UJENZI,UKARABATI WA VIWANJA:- Wakati wa utawala  wa  Rais   Samia   unaingia  madarakani    uliahidi  utatenga  bajeti  ya  fedha  kwa  ajili  ya  kusaidia maboresho  ya  viwanja    vya  soka  katika maeno mbalimbali nchini (Rejea marekebisho/maboresho ya uwanja wa Benjamini Mkapa ambao kiasi cha shilingi bilioni 31 zinakadiriwa kuuboresha uwanja huo)
KUTOA NDEGE KWA TIMU YA YANGA :- Mei 2023 Mhe Rais Dkt Samia alitoa ndege  binafsi (Boeing 787-8 Dreamliner ) kwa ajili ya kupeleka timu, viongozi na mashabiki wa timu  ya Yanga  katika hatua ya fainali ya Kombe la Shirikisho  Afrika waliyocheza na  Algers USM Alger ya  Algeria tarehe 3 Juni, 2023
MHE.RAIS DKT SAMIA KUWA MGENI RASMI,SIMBA DAY :-Agosti 6  Mwaka 2023 Mhe Rais Dkt Samia Suluhu alikubali kuwa mgeni rasmi kwenye tamasha la Simba Dat lililofanyika katika uwanja wa Benjamin Mkapa
KUANDAA AFCON 2027 :- Uongozi  wa  Rais  Samia  ulianzisha   wazo  la kuomba   kuandaa fainali za mataifa ya Afrika (Afcon) mwaka  2027, Kutokana na hilo, ilishauriwa  kwamba ni vyema Tanzania ingeomba kuandaa kwa  pamoja  mashindano  hayo  na nchi za  Kenya na Uganda ambazo ipo nazo pamoja  katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, lakini  pia  ni  wanachama wa baraza la vyama vya mpira wa miguu  Afrika  Mashariki na Kati(Cecafa).
TWIGA STARS KUFUZU KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA KWA WANAWAKE CAF 2024 :- Mafanikio mengine makubwa katika maendeleo ya michezo yamefikiwa na timu ya taifa ya wanawake ya wakubwa, Twiga Stars, ilipofuzu kwa mara ya kwanza kushiriki michuano ya CAF Women’s Africa Cup of Nations (WAFCON) 2024, itakayofanyika mwaka huu huko Nchini Morocco
#DktSamiamiakamitatuMichezoni