MANISPAA YA SINGIDA BARABARA ZIPO SAFI
SINGIDA
Utekelezaji wa miradi ya barabara katika Halmashauri ya Manispaa ya Singida upo katika hali nzuri kwa 75% na Manispaa hiyo ina jumla ya mtandao wa barabara wenye urefu wa Km 523.
Aidha serikali kupitia TARURA kwa sasa inatekeleza miradi miwili ya ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami eneo la Mnung’una na ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami eneo la Mwenge-Mungumaji ambapo kaisi cha shilingi bilioni 2.7 kimetengwa.
Chanzo:-Meneja wa TARURA Mkoa wa Singida, Eng. Ibrahimu Kibasa
Serikali kupitia TARURA itaendelea kuboresha barabara za Manispaa na Halmashauri nyinginezo kwa kuhakikisha zinakuwa katika ubora kwa kiwango cha lami, changarawe na kujenga madaraja katika maeneo mbalimbali yaliyo na changamoto.
