KANDA YA ZIWA KUWA NA VITUO VIWLI HUDUMA BOBEZI YA MOYO
GEITA
Serikali kupitia Wizara ya Afya imedhamiria kuifanya Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Chato kuwa kituo cha umahiri wa matibabu ya ubingwa na ubingwa bobezi wa moyo ili kuipa nguvu hospitali ya kanda ya Bugando.
Kanda ya Ziwa ina watu takribani milioni 22, hivyo serikali imeona ipo haja ya kuwa na Hospitali ya Rufaa ya Kanda nyingine katika ukanda wa ziwa(Mwanza, Geita, Simiyu, Shinyanga, Kagera pamoja na Kigoma na ianze kutoa huduma za matibabu ya ubingwa na ubingwa bobezi wa moyo katika ukanda huo wa ziwa.
Kwa hatua hii, huduma za magonjwa ya moyo za watu wa Kanda ya ziwa zitaishia Chato ili kurahisisha upatikanaji wa huduma hizo karibu na wananchi pamoja na kupunguza msongamano wa wagonjwa wa moyo JKCI – Dar es Salaam.
