TSH TRILIONI 2.5 KUBORESHA RELI YA TAZARA

 

TSH TRILIONI 2.5 KUBORESHA RELI YA TAZARA

TSH TRILIONI 2.5 KUBORESHA RELI YA TAZARA

ZAMBIA
Jumla  ya Shilingi trilioni 2.5 ( Dola 1 bilioni za  Marekani)zinatarajiwa  kutumika kwa ajili 
ya matengenezo ya reli ya  Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (Tazara), yenye umri wa karibu miongo mitano sasa.
Taarifa kuhusu gharama  za maboresho ya reli hiyo, imetolewa na Balozi wa China nchini Zambia, Du Xiaohui, hivi karibuni.
Reli hiyo inayounganisha Bandari ya Dar es Salaam na Mji wa Kapiri Mposhi nchini Zambia  ni  miongoni mwa miradi  ambayo China ilifadhili  ujenzi wake uliokamilika  mwaka 1975.Mapema wiki iliyopita, Xiaohui aliwasilisha pendekezo la mradi wa matengenezo ya reli hiyo  kwa Waziri wa  Usafirishaji wa Zambia, Frank Tayali.