TSH BIL 700 ZAJENGA GHALA ZA MAZAO NCHINI

 

TSH BIL 700 ZAJENGA GHALA ZA MAZAO NCHINI

TSH BIL 700 ZAJENGA GHALA ZA MAZAO NCHINI

DAR ES SALAAM 
Katika kuendelea kuboresha wizara ya kilimo, serikali ya awamu ya sita kupitia wizara tajwa  imetumia kiasi cha shilingi bilioni 700 kukamilisha ukarabati na ujenzi  wa ghala na vihenge katika maeneo mbalimbali nchini. 
Wizara kupitia CPB imekamilisha ukarabati wa ghala la Kiteto Mkoani Manyara (tani 1,000); Mbugani Mkoani Dodoma (tani 30,000) na vihenge Mkoani Arusha (tani 38,000). 
Aidha, hadi Aprili, 2022 ukarabati wa ghala tisa (9) katika Halmashauri za Wilaya za Songea na Madaba umefikia hatua mbalimbali kama ifutavyo: Songea DC - Mkongotema (89.5), Muungano Zomba (64.74), Litisha (48.67), Magagura (55.09), Lipaya (21.58); Madaba DC - Hagangadinda (57.8), Matetereka (45.13) Lilondo B (83.5) na Gumbiro (96.28). Ukarabati huo unahusisha sakafu, kuta, paa, vyoo na kuweka mfumo wa maji.