TANZANIA,CHINA KUBORESHA USHIRIKIANO HUDUMA ZA MATIBABU

 

TANZANIA,CHINA KUBORESHA USHIRIKIANO HUDUMA ZA MATIBABU

TANZANIA,CHINA KUBORESHA USHIRIKIANO HUDUMA ZA MATIBABU

DAR ES SALAAM
Tanzania na China zinachunguza uwezekano mpya wa kuimarisha ushirikiano wa kibiashara ili kuboresha huduma za afya.
Katika kipindi cha miongo sita iliyopita, serikali ya China imetuma takriban wajumbe 1,500 wa timu za madaktari kusaidia kuboresha huduma za afya kwa watu nchini Tanzania. 
Madaktari hao inakadiriwa kuwa wameokoa maisha ya zaidi ya Watanzania milioni 20 wanaougua. Wataalamu hao wa China pia wamekamilisha uchunguzi wa karibu 15,000, wamefanya upasuaji zaidi ya 3,000, walishiriki katika karibu hatua 2,000 za huduma muhimu, kudhibiti anesthesia kwa zaidi ya 7,000.