DKT SAMIA AADHIMISHA SIKU YAKE YA KUZALIWA KWA KUPANDA MITI
ZANZIBAR
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ameitumia siku yake ya kuzaliwa kwa kushiriki zoezi la upandaji miti katika eneo la Donge Muwanda Visiwani Zanzibar leo tarehe 27 Januari 2024.
Pamoja na zoezi la upandaji miti Dkt Samia amekata keki ikiwa ni njia ya kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa leo tarehe 27, Januari.
Akizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye zoezi hilo la upandaji miti visiwan Zanzibar amewataka wakazi hao kuendelea kupanda mingi na kuitunza pia amewaagiza viongozi wa serikali kuhakikisha wanazuia shughuli za uchimbaji mchanga kiholela katika eneo la Donge Muwanda.
#HAPPYBIRTHDAYBIMKUBWA.