WAWEKEZAJI 901 WAWEKEZA NCHINI MWAKA 2024

 

WAWEKEZAJI 901 WAWEKEZA NCHINI  MWAKA 2024

WAWEKEZAJI 901 WAWEKEZA NCHINI  MWAKA 2024

TANZANIA
Kituo Cha Uwekezaji Nchini (TIC) kwa mwaka 2024 kimefanya usajili wa miradi ya wawekezaji  901 kutoka miradi 500 ya mwaka 2023 ongezeko ambalo ni sawa na asilimia 44.5.
Miradi 500 ya uwekezaji iliyosajiliwa mwaka 2023 ina thamani ya dola za kimarekani bilioni tano (sawa na shilingi 1,253,750,000,000) huku miradi 901 iliyosajiliwa mwaka 2024ina thamani ya dola za kimarekani bilioni 9.3 ( shilingi 2,331,975,000,000)
Mafanikio  hayo yametokana na uboreshaji wa mazingira bora ya uwekezaji pamoja  na mabadiliko ya uwekezaji mwaka 2022 ambayo imeondoa vikwazo vingi kwenye usajili wa uwekezaji,pia kwa sasa TIC ina kituo cha One Stop Center ambapo  usajili wa miradi huduma zote hupatikana sehemu moja na ukamilishaji unafanyika ndani ya siku tatu pekee.