SH TRIL. 11.4 KUTEKELEZA MIRADI KIGOMA
KIGOMA
Kwa kipindi cha uongozi wa awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Serikali imepeleka shilingi trilioni 11.4 mkoani Kigoma kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya wananchi.
Baadhi ya matumizi ya fedha hizo ni utekelezaji miradi ya umeme kiasi cha sh bilioni 534 ikiwemo umeme wa gridi ya Taifa kutoka Nyakanazi shilingi Bilioni 467.3 na uzalishaji wa umeme wa maporomo ya Igamba shilingi bilioni 66.7 huku kiasi kingine cha fedha kikienda kwenye miradi mingine ya maendeleo
