TSH BIL 3 ZAJENGA HOSPITALI YA WILAYA MISUNGWI

 

Ilikuwa ni Juni 14,2023 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe,Dkt Samia Suluhu Hassan katika ziara yake akizungumza na wananchi katika eneo la Kigongo alipotoa ahadi ya  kununua vifaa Vifaa tiba kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya ya Misungwi  ili kuwezesha Wananchi kupata huduma bora za Afya Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

TSH BIL 3 ZAJENGA HOSPITALI YA WILAYA MISUNGWI

MWANZA
Serikali ya awamu ya sita imeidhinisha kiasi cha shilingi bilioni 3.5 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya wilaya Misungwi iliyojengwa katika kijiji cha Iteja Mkoani Mwanza.
Kiasi hicho cha fedha kimefanikisha ujenzi wa majengo zaidi ya 14, kukamilika kwa hospitali hiyo kumewarahishia wananchi wa maeneo hayo ambao hapo awali walilazimika kuifata kwenye kituo cha Afya Mitindo kilicho umbali wa Kilomita 8.