TANZANIA NA RWANDA KUSHIRIKIANA SEKTA YA MAZIWA
DODOMA
Tanzania na Rwanda zimetiliana saini Mkataba wa Makubaliano (MoU) ili kuinua sekta ya maziwa, kuashiria juhudi za ushirikiano kati ya nchi hizo mbili wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Mkataba huo umetiwa saini na Wizara ya Mifugo na Uvuvi ya Tanzania na Rwanda, Jenerali (Mst.) James Kabarebe, anayeshughulikia Mambo ya Nje.
Ushirikiano huo unalenga kutengeneza fursa nyingi za ajira kwa wananchi na kuongeza utoaji wa lishe ambapo nchi zote mbili zitaongeza juhudi katika uzalishaji na usindikaji wa maziwa.