RAIS WA NAMIBIA MHE. DKT NETUMBO NANDI-NDAITWAH KUFANYA ZIARA NCHINI

 

RAIS WA NAMIBIA MHE. DKT NETUMBO NANDI-NDAITWAH KUFANYA ZIARA NCHINI

RAIS WA NAMIBIA MHE. DKT NETUMBO NANDI-NDAITWAH KUFANYA ZIARA NCHINI

DAR ES SALAAM
Rais wa Jamhuri ya Namibia Mhe. Netumbo Nandi-Ndaitwah anatarajia kufanya ziara ya kiserikali ya siku mbili  nchini Tanzania kuanzia (leo) Mei 20 hadi 21, 2025 kufuatia  mwaliko aliopewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Hii ni ziara ya kwanza ya Mhe. Nandi-Ndaitwah kuifanya  hapa nchini tangu alipoapishwa kuwa Rais wa Namibia tarehe 21 Machi  2025 na inalenga kukuza ushirikiano wa kisiasa, kiuchumi na kijamii ikiwemo katika nyanja za kibiashara, uwekezaji na elimu.
Tutakuletea matangazo ya moja kwa moja , tufuatilie kwenye mitandao yetu yakijamii facebook, x, instagram, Tiktok na Youtube @Bimkubwatanzania.