ZIARA YA DKT SAMIA KOREA YALETA KAMPUNI 38 NCHINI
DAR ES SALAAM
Ziara aliyoifanya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan mwezi Juni mwaka huu nchini Korea imezaa matunda baada ya makampuni 38 kutoka Korea kuja nchini na kuungana na mengine 50 Ya Tanzania kwa nia ya kufanya uwekezaji wa ubia katika maji, miundombinu, mafuta, gesi na madini nchini Tanzania.
Mhe.Rais Dkt Samia katika ziara yake ya kihistoria nchini Korea aliibua fursa za kiuchumi za Tanzania katika maeneo mbalimbali, ikiwa ni pamoja na nishati ambayo wawekezaji wa Korea wangeweza kuingiza mitaji yao kupitia ubia na wawekezaji wa ndani.
Kaa nasi kwa taarifa zaidi.
