TSH BIL 1.7 KUMALIZA KERO YA MAJI KATA YA KITULA , MBINGA

 

TSH BIL  1.7 KUMALIZA KERO YA MAJI KATA YA KITULA , MBINGA

TSH BIL  1.7 KUMALIZA KERO YA MAJI KATA YA KITULA , MBINGA

RUVUMA
Serikali kupitia wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini(Ruwasa)wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma,umeanza kutekeleza mradi wa maji ya bomba wa Kitula kata ya Kitula Halmashauri ya wilaya Mbinga utakaowaondolea  wananchi wa kata hiyo kero ya kuamka usiku wa manane na kutembea umbali mrefu  kila siku kwenda kutafuta maji na kuacha shughuli  za kujipatia kipato.
Mradi wa maji Kitula unatekelezwa kwa gharama ya Sh.bilioni 1.7 na utawanufaisha wananchi  9,100 wa vijiji  vinne vya Mzuzu,Kitula,Mahilo na Lisau  na utekelezaji wake umefikia zaidi ya 85%.
Hadi sasa kazi zinazofanyika katika mradi huo ni ujenzi wa matenki matatu moja  la lita 150,000  la pili la ujazo wa lita 100,000 la tatu lina uwezo wa kuhifadhi lita 75,000 na kulaza mabomba  urefu kilometa 54.