MABWAWA KWA AJILI YA MIFUGO YAJENGWA
ARUSHA
Katika mwaka 2023/2024, serikali kupitia Wizara ya uvuvi na mifugo kwa kushirikiana na Mamlaka za Serikali za Mitaa imefanikiwa kuendelea kuimarisha upatikanaji wa maji kwa mifugo ambapo imekamilisha ujenzi wa mabwawa matatu (3) ya Kongwa (Dodoma), Naalarami (Monduli) na Vinyenze (Kibaha).
Mabwawa hayo yanakadiriwa kuhifadhi wastani wa lita milioni 100 za maji na yana uwezo wa kunywesha mifugo 3,500 kwa siku kila moja.