TSH BIL 70.8 KUJENGA BARABARA MLIMBA DC

 

TSH BIL 70.8 KUJENGA BARABARA MLIMBA DC

TSH BIL 70.8 KUJENGA BARABARA MLIMBA DC

MOROGORO
Kiasi cha shilingi bilioni 70.8 kimetolewa na serikali ya awamu ya sita kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Mbingu-Chita Km 37.5 kwa kiwango cha lami iliyopo Halmashauri ya wilaya Mlimba Mkoani Morogoro .
Ujenzi wa barabara hiyo umeanza Juni 25, 2024 na unatarajiwa kutekelezwa ndani ya miezi 20 kuanzia siku ulipokabidhiwa.