TANZANIA KUWA MWENYEJI WA WAKUU WA ANGA BARANI AFRIKA

 

TANZANIA KUWA MWENYEJI WA WAKUU WA ANGA BARANI AFRIKA

TANZANIA KUWA MWENYEJI WA WAKUU WA ANGA BARANI AFRIKA

ARUSHA
Wakuu wa usafiri wa anga kutoka kote barani Afrika wanakutana mjini Arusha, Tanzania  tarehe 6 juni 2024 ili kujadili mikakati bunifu ya kukuza sekta ya usafiri wa anga barani humo.
Kufuatia Tanzania kuandaa  hafla hiyo, Rais wa Kamisheni ya Usafiri wa Anga ya Afrika, Mhe. Silas Udahemuka, ametoa shukrani zake kwa Tanzania kwa kuandaa hafla hiyo  huku  akiwataka wajumbe kuchangamkia fursa hiyo kutatua na kuondokana na changamoto za sekta hiyo kwa njia ya mazungumzo yenye kujenga.
Mkutano huo wa utakaofanyika katika Hoteli ya Gran Melia jijini Arusha, utahusisha pia kutembelea Hifadhi ya Ngorongoro ikiwa pia ni sehemu ya juhudi za kukuza utalii nchini Tanzania, na kuongeza mwelekeo wa kitamaduni na mazingira katika hafla hiyo.
Taarifa kutoka  Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAAimesisitiza  kuwa mkutano huo sio tu wa kutatua changamoto. Pia inahusu kuunda sauti ya umoja wa Kiafrika katika vikao vya kimataifa, kuhakikisha maslahi ya usafiri wa anga ya bara hili yanawakilishwa vyema na kulindwa.