RIPOTI:-TANZANIA YATAJWA NCHI YENYE DEMOKRASIA DUNIANI

 

RIPOTI-TANZANIA YATAJWA NCHI YENYE DEMOKRASIA DUNIANI

RIPOTI-TANZANIA YATAJWA NCHI YENYE DEMOKRASIA DUNIANI

UINGEREZA

Tanzania imetajwa kuwa ni miongoni mwa nchi zenye demokrasia safi ulimwenguni huku ikishika nafasi ya kwanza kwa nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki(EAC).Ripoti   ya   hali   ya   demokrasia   duniani   iliyoandaliwa   na   Economist  Intelligence  Unit  (EIU)  kupitia   ripoti   yake   ya   “Democracy  Index   2023”   imeangazia   hali   ya   demokrasia katika nchi 165 ambapo Vigezo    vilivyotumika    kupima    hali  ya  demokrasia  katika  mataifa  hayo vimezingatia mambo kadhaa, ikiwemo mchakato wa uchaguzi na mfumo  wa  vyama  vingi,  utendaji  kazi  wa  Serikali,  ushiriki  wa  kisiasa, utamaduni wa kisiasa na uhuru wa wananchi.

Kwa kuzingatia vigezo   hivyo,   kila  nchi  inawekwa kwenye  kundi  lake   kati   ya   makundi   manne   ya   utawala   ambayo   ni   demokrasia   kamili, demokrasia yenye upungufu,  utawala  mseto  na  utawala  wa  kiimla. 

Kwa  upande  wa  alama, Tanzania  inaongoza  katika  nchi  za  Afrika   Mashariki   ikishika   nafasi   ya   12   kikanda   na   kidunia   nafasi   ya   86,  ikifuatiwa  na  Kenya  nafasi  ya  14  kikanda  na  92  kidunia  wakati  Uganda inashika nafasi ya 16 kikanda na 99 kidunia

MAONI YA WADAU KUHUSU NAFASI HII YA TANZANIA

Mwanazuoni  wa sayansi ya siasa na sheria kutoka Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria   kwa   Vitendo   (LST),   Profesa   Ambrose Kessy   anasema   nafasi   ya   Tanzania   kwenye   ripoti hiyo si  jambo  la  kushangaza  kwa  sasa  kutokana  na  Rais  aliyepo  madarakani (Samia Suluhu Hassan).

“Serikali   ya   sasa   imebadilika,   imetoa  uhuru  mkubwa  kwa  watu  kujieleza   bila   kuvunja   sheria   na   nafikiri   imejitathimini   na   kuona   kila  mtu  anayo  nafasi  ya  kufanya  mapinduzi  katika  taifa  iwapo  atapewa nafasi,” anasema Kessy.

Kessy amaeongeza “Rais Samia amejitahidi kufanya mengi  na  yote  hayo  yanaonekana  ni  katika  kuionesha  dunia  tunakua  kutoka   chini   ambako   watu   walikuwa  wanalalamika  kutokuwa  na  uhuru  hasa  vyama  vya  upinzani,” 

Nae, Dkt  Paul  Loisuilie Mhadhiri  wa Chuo Kikuu cha  Dodoma   (Udom) anasema 4R imechangia kwa kiwango   kikubwa   katika   kipindi  hiki na imesaidia kuleta mapinduzi ya siasa za Tanzania,

 “Ndani  ya  kipindi  hiki  ustahimilivu  umeshamiri kwa kiwango kikubwa kwa viongozi wa kiserikali,kitendo  cha  kuacha  uhuru  wa  watu  kupumua  kusema  ya kwao imeleta ufanisi mkubwa.Pia  hata  Rais  mwenyewe  anaonesha  utashi  mkubwa  wa  kisiasa,  anastahimili  vya  kutosha  kwa  kuamini  nchi  inapaswa  kujengwa  na  wote  kwa  kuruhusu  kila  mmoja  kutoa mawazo yake,” anasema.

Amesisitiza kwamba  ndani  ya  kipindi  cha  miaka  miwili  nyuma  Serikali  imekuwa  ikifanya  maridhiano  na  vyama  vya  siasa  na  utulivu  unazidi  kuongezeka   na   ni   eneo   ambalo   hata Kenya wamezidiwa.

#PumzikaKwaAmaniMzeeMwinyi