TSH TRIL 1 ZABORESHA ELIMU NCHINI
DODOMA
Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt Samia Suluhu Hassan imetumia Sh trilioni 1.29 kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia nchini
Aidha Shilingi bilioni 454.3 zimetolewa na serikali kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya shule za elimu ya awali na msingi ambapo jumla ya shule mpya 346 zimejengwa, vyumba vya madarasa 9,189, nyumba za walimu 346, mabweni 28 na ukarabati wa shule kongwe 45.
