TEMEKE NA MKURANGA KUUNGANISHWA NA DMDP
DODOMA
Wilaya ya Temeke iliyopo Mkoa wa Dar es salaam na wilaya ya Mkuranga ya Mkoa wa Pwani zinatarajiwa kuunganishwa kwa kujenga madaraja/makaravati ya Churwi,Tabowa na Majimatitu kupitia mradi wa uendelezaji wa Jiji la Dar es Salaam (DMDP).
Aidha mpaka sasa maeneo matatu ya Kilwa, Tambani na Rufu Nampombo yameunganishwa kwa madaraja/makalavati na yanapitika kwa mwaka mzima.
