DAR YAPEWA TSH BIL 52 KUIMARISHA SEKTA YA AFYA

 

DAR YAPEWA TSH BIL 52 KUIMARISHA SEKTA YA AFYA

DAR YAPEWA TSH BIL 52 KUIMARISHA SEKTA YA AFYA

DAR ES SALAAM
Serikali imeupatia mkoa wa Dar es salaam kiasi cha shilingi  bilioni 52  kwa ajili ya kuimarisha sekta ya afya na hadi sasa fedha hizo zinajenga  vituo vipya vya afya, uboreshoji wa miundombinu, vifaa tiba, utoaji huduma huku utekelezaji wa miradi mingine mipya ukiendelea.
Uwekezaji huo unaofanywa na serikali ya awamu ya sita katika sekta ya afya umeleta mapinduzi makubwa ya utoaji huduma kwa wananchi.