JUZUU MPYA ZA SHERIA KURAHISIHA MAAMUZI MAHAKAMANI

 

JUZUU MPYA ZA SHERIA KURAHISIHA MAAMUZI MAHAKAMANI

JUZUU MPYA ZA SHERIA KURAHISIHA MAAMUZI MAHAKAMANI

DODOMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan  amesema juzuu mpya za toleo la Sheria za Tanzania zilizofanyiwa urekebu la mwaka 2023 zitasaidia katika kurahisisha maamuzi mahakamani,kuongeza uwazi hatua ambayo itaongeza kujenga imani ya wananchi kwa serikali yao.

Akizungumza  mara baada ya kutia saini  Tamko la kuzindua Toleo la Sheria za Tanzania zilizofanyiwa urekebu la mwaka 2023 kwa mujibu wa kifungu cha 12 cha Sheria ya urekebu wa sheria  Dkt Samia amesema

" kwa upande wa mahakama tunatazamia itapunguza muda unaotumika kwenye kufanya utafiti ili kupata uhakika wa sheria inavyosema na hivyo kurahisisha maamuzi"

 Dkt Samia ameongeza "Juzuu hizi za sheria zilizorekebishwa ni muhimu sana katika kuongeza uwazi na kuzidi kujenga imani ya wananchi kwa serikali yao,aidha ni nyenzo muhimu itakayosaidia kupunguza matumizimabaya yamadaraka"

ZINGATIA:- ZOEZI LA UZINDUZI WA UREKEBU WA SHERIA UMEJUMUISHA SHERIA ZOTE ZILIZOTUMIKA KUANZIA MWAKA 2003  HADI DESEMBA 2023 NA SHERIA ZOTE  KUU 446 ZIMEHUSISHWA KWENYE MABADILIKO HAYA YALIYOZINDULIWA APRIL 23,2025