SERIKALI IMEIMAIRISHA MIUNDOMBINU MOROGORO

 

SERIKALI IMEIMAIRISHA MIUNDOMBINU MOROGORO

SERIKALI IMEIMAIRISHA MIUNDOMBINU MOROGORO

MOROGORO
Serikali ya awamu ya sita inaendelea kutekeleza miradi mikubwa ya Kitaifa Mkoani Morogoro ikiwemo Ujenzi wa Barabara ya Mikumi - Kidatu – Ifakara (sehemu ya Kidatu – Ifakara, (km 66.9) kwa kiwango cha lami pamoja na ujenzi wa Daraja la Ruaha Mkuu ambao umefikia asilimia 86% za utekelezaji na tayari Mkandarasi amekamilisha km 55.67 za lami kati ya km 66.9 zinazotakiwa kwa mujibu wa Mkataba.
 Pia inaendelea na Ujenzi wa barabara ya Dumila – Kilosa – Mikumi (km 142) kwa kiwango cha lami (sehemu ya Rudewa – Kilosa km 24) kwa kutumia fedha za ndani; Mkandarasi amekamilisha ujenzi wa kilometa 22.05; barabara imekabidhiwa na inatumika, Mkandarasi amekamilisha pia madaraja matatu ya Kobe, Wailonga na Mazinyungu na kwasasa anaendelea na kazi ya km 0.75 ya maungio ya madaraja hayo.
#HodiMorogoroTwakusaaho