TSH BIL 36 ZAJENGA TAWI LA MUHAS KIGOMA
KIGOMA
Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imetumia kiasi cha shilingi bilioni 36 kwa ajili ya ujenzi wa tawi la chuo kikuu cha afya cha Muhimbili (MUHAS), ujenzi, ukarabati na uboreshaji wa miundo mbinu ya afya ya mkoa wa Kigoma na kutumia sh bilioni tano kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya rufaa ya kanda.
